RECAP: Diamond anatoa somo uwekezaji kwenye video – El Mando
Kupitia kwenye kipindi chake cha RECAP & MANDO @el_mando_tz ameizungumzia video mpya ya
Diamond Platnumz akiwa na Bien kutoka Kenya ya KATAM.
Anasema Diamond bado anaendelea kuwa Mfano kwenye vitu vingi sana hasa kwa wasanii wa hapa nyumbani Tanzania.
Anasema, asilimia kubwa ya wasanii Bongo hawawekezi tena kwenyw video bali wanafanya Vide Lyrics au Visualizer basi.
Kama msanii anafanya video basi ujue kwa kiwango kikubwa video itakuwa yakawaida sana Tofauti na Diamond.
Hata kwenye nyimbo alizoshirikishwa mfano OLOLUFE MI na
Jux, SALAMA na Barnaba, NESA NESA na Rayvanny pia ngoma zake kama KOMASAVA na hii KATAM unaona kabisa Quality ya Video uwekezaji umewekwa.
Anasema bado msimamo wake upo pale pale, Collabo ya Bien na Diamond ya kawaida kwa level zao na ukubwa wao, wangetakiwa watupatue Collabo bora ya mwaka.
Uchambuzi mzima upo katika akaunti yetu ya YouTube ya Bongofive.
Cameraman @samirkakaa






