Burudani
RECAP: Majizzo ameheshimisha Bongo Fleva – El Mando

Kupitia kwenye kipindi chake cha RECAP & MANDO @el_mando_tz amezungumzia namna Jukwaa la Samia Festival lilivyoweka historia Tanzania.
Anasema Majizzo kwa sasa ni Godfather kwenyw Biashara ya Burudani Tanzania, ameshika sehemu kubwa sana na anategemewa kwenye maeneo makubwa mno.
Lazima apongezwe kwa mapinduzi anayoyafanya kwa kufunga Jukwaa lenye hadhi ya Coachella au Rolling Loud katika ardhi ya Tanzania.
Anaongeza kuwa, ili muziki wetu upige hatua hatuwahitaji wasanii pekee yao bali tunahitaji kundi kubwa sana la watu watakaoifanya biashara ya muziki Tanzania ifanikiwe.
Uchambuzi mzima upo katika akaunti yetu ya YouTube ya Bongofive.
Cameraman @samirkakaa