Bongo5 ExclusivesFahamuHabariSiasa

Saa ya Hitler iliyouzwa dola milioni 1.1 mnadani, yauzwa tena

ALEXANDER HISTORICAL AUCTIONS

Saa ya mkononi iliyosemekana kuwa ni ya aliyekuwa kiongozi wa Wanazi Adolf Hitler imeuzwa kwa dola milioni 1.1 katika mnada  nchini Marekani.

Saa hiyo, inayoitwa Huber Timepiece, iliuzwa kwa mnunuzi ambaye hajuliikani. saa hiyo imeandikwa Herufi -AH ( kwa kirefu-Adolf Hitler).

Mauzo ya saa hiyo yalipingwa na viongozi wa Kiyahudi kabla ya Mnada huo wa Kihistoria kufanyika -Alexander Historical Auction huko Maryland.

Hatahivyo, kampuni iliyonunua iliviambia vyombo vya habari vya Ujerumani kwamba walikuwa wanajaribu kutunza historia.

Adolf Hitler aliiongoza Ujerumani chini ya utawala wa Nazi kuanzia mwaka 1933 hadi 1945.Watu zaidi ya milioni waliuawa kikatili wakati wa utawala wake. huku ikielewa kuwa zaidi ya Watu laki sita kati yao waliuawa tu kwasababu walikuwa ni Wayahudi.

ALEXANDER HISTORICAL AUCTIONS

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents