Klabu ya Al Ahly imeripotiwa kuwa imepanga ofa nono ikinuwia kutaka kumsajili Mshambuliaji wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta kwenye dirisha hili la mwezi Januari.
Al Ahly inatafuta mshambuliaji wakati ambapo ilihusishwa na mchezaji wa DR Congo, Jackson Muleka hata hivyo ofa yao imegonga mwamba mbele ya Besiktas.
Inadaiwa hiyo ndiyo sababu ya Al Ahly kumgeukia nahodha wa wa Tanzania Mbwana Samatta kama ndiyo tageti yao iliyobaki kipindi hiki cha dirisha la Januari.
Imeandikwa na @fumo255