Sikurudi Man United kuwania ‘Top Four’, wala kucheza Europa League – Ronaldo
Mchezaji wa klabu ya Manchester United, Cristiano Ronaldo amesema kuwa wananapaswa kupambana kuhakikisha timu hiyo inakuwa ndani ya tatu bora ya msimamo wa ligi mwisho wa msimu na kusisitiza kutokuwa kwenye nafasi hiyo kutakuwa ni kufeli.
Ronaldo amesema kuwa hajaondoka Juventus kuja kupambania nafasi ya nne ”Manchester United inapaswa kutwaa ubingwa wa Ligi, kushika nafasi ya pili au ya tatu.”
”Sioni nafasi nyingine kwa Manchester United kuwa mkweli sioni nafasi nyingine. Sitaweza kukubali uwezo wetu kubaki nje ya tatu bora kwenye Premier League.”
Ronaldo anaamini kuwa anaamini wanayonafasi ya kuwania ubingwa tangu alivyorejea Old Trafford kipindi cha majira ya joto kilichopita, lakini hata hivyo United tayari imezidiwa jumla ya point 22 kutoka kwa vinara wa Ligi Manchester City huku wakishika nafasi ya saba (7).
Mchezaji huyo mwenye mafanikio makubwa kunako mchezo wa mpira wa miguu, Ronaldo ambaye mpaka sasa ameshafunga magoli 14 kwenye michezo 21 amesema kuwa kocha wake Mjerumani Ralf Rangnick anafanya vizuri isipokuwa anahitaji apewe muda.
IMEANDIKWA NA @fumo255