Michezo

Simba inakwenda kutetea ubingwa wake – Mwenyekiti wa Bodi Abdallah Muhene “Try Again”

Mwenyekiti wa Bodi ya Klabu ya Simba, Salim Abdallah Muhene “Try Again” amewahakikishia mashabiki, wapenzi na wanachama timhu hiyo kuwa wanakwenda kuutetea Ubingwa wao kwa mara ya tano mfululizo huku akijinasibu kuwa nia wanayo, nguvu nawazo na pesa pia wanazo.

“Nataka niwambie Simba inakwenda kutetea tena ubingwa wake, hilo hakuna shaka kabisa. Nia tunayo, uwezo tunao, nguvu tunayo, pesa tunazo. Nini cha kutuzuia?”- Mwenyekiti wa Bodi, Salim Abdallah Muhene “Try Again”.

Ligi ya Msimu huu 2020/21 inaonekana kuwa ngumu zaidi ukilinganisha na msimu uliyopita hasa kutokana na kuimarika kwa mtani wao Yanga SC na baadhi ya timu chache ambazo zimeonekana kuleta ushindani mkubwa kwa bingwa mtetezi Simba SC,

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents