HabariMichezo

Simba tupo tayari vs Raja CA- Murtaza Mangungu

Mwenyekiti wa Klabu, Murtaza Mangungu amesema kuwa wameshafanya maandalizi kwaajili ya kumvaa Raja Casablanca Jumamosi ya Februari 18, 2023 Benjamin Mkapa.

”Maandalizi yote yanayotakiwa kufanyika ndani na nje ya uwanja yamefanyika, lengo letu ni kuhakikisha mashabiki wanaujaza uwanja wote wa Benjamin Mkapa.”-Mwenyekiti Murtaza Mangungu

Mangungu ameongeza ”Sio mara ya kwanza kucheza mechi kubwa kama hii, wachezaji wanajua umuhimu wa mchezo huu. Ilitokea bahati mbaya tukapoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Horoya ugenini hilo hatutaki lijirudie tena.”

Murtaza Mangungu ameyasema hayo wakati wa Uzinduzi wa kampeni ya hamasa kuelekea huo wa pili wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Raja Casablanca ya Morocco.

Credit @fumo255

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents