HabariMichezo

Simba wakutana na rungu la TFF

KAMATI ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Disemba 1, 2022 ilipitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kufanya maamuzi yafuatayo;

Mechi Namba 37: Mbeya City FC 1-1 Simba SC

Timu ya Simba imetozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la baadhi ya wachezaji wake kuingia uwanjani kwa kupitia mlango usio rasmi kuelekea mchezo tajwa hapo juu uliofanyika kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya Novemba 23, 2022.

Simba walilazimisha baadhi ya wachezaji wao waruhusiwe kuingia uwanjani kupitia mlango wa kuingilia jukwaa la watu maalum na walipozuiwa na walinzi wa uwanjani (stewards), Simba walitumia nguvu kutimiza nia yao.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 17:(21 & 60) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mchezaji wa timu ya Simba, Gadiel Michael amefungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kulazimisha kuingia uwanjani saa 4:25 asubuhi ya siku ya mchezo tajwa hapo juu kwa kile alichoeleza alitaka kukagua kiwanja.

Licha ya walinzi wa uwanja huo kumzuia Gadiel (ambaye alikuwa ameongozana na watu kadhaa waliovalia fulana zenye nembo ya klabu ya Simba), kwasababu haukuwa muda rasmi kwa ajili ya zoezi hilo na Simba hawakufanya mawasiliano yoyote na Kamishna wala Mratibu wa Mchezo wakieleza jambo hilo, Gadiel alitumia hila na kufanikiwa kuwakwepa walinzi hao kisha kuingia kiwanjani.

Mchezaji huyo alipoingia kiwanjani hakuonesha dalili yoyote ya kukagua eneo la kuchezea na badala yake alionekana kwenda moja kwa moja hadi eneo la katikati ya kiwanja na kumwaga vitu vyenye asili ya unga.

Adhabu hii ni kwa uzingativu wa Kanuni 41:5(5.5) ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti kwa Wachezaji.

 

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents