Msanii wa Bongo Fleva, @staminashorwebwenziameibuka kidedea baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa Tuzo ya PSMA katika kipengele cha Msanii Bora wa Hip Hop/Rap katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Tuzo hizo zimetolewa usiku wa kuamkia juzi Jumamosi katika Jiji la Bujumbura, Burundi na kuwashirikisha wasanii kutoka nchi mbalimbali za Afrika Mashariki.
Kupitia Instagram yake Stamina ameandika kuwa.
”
Napenda kutoa shukrani za dhati kwa mashabiki zangu wote walionipigia kura na wadau waliosupport bila kuwasahau waandaaji wenyewe @platformshow257
Ushindi umerudi nyumbani TANZANIA…na sasa ni MSANII BORA WA RAP/HIP HOP WA AFRIKA MASHARIKI katika TUZO ZA @platformshow257 za nchini BURUNDI
JIWE WALILOLIKATAA WAASHI LIMEKUA JIWE KUU LA PEMBENI😂💪
Ahsanteni sana🙏”