Bongo5 ExclusivesHabariMahojianoMichezo
Tambo za mashabiki wa Simba wakiwatania watani wao Yanga baada ya jezi kutambulishwa
Siku ya leo klabu ya Simba umetambulisha jezi zake na mashabiki wa klabu hiyo wamekuwa na mwitikio mkubwa juu ya kununua jezi za klabu yao.
Wakiwa wamefurika nje ya duka la Vunja Bei wakiwa kwenye foleni imeonyesha namna gani mashabiki wa klabu hiyo walikuwa wanazisubiria jezi kwa hamu kubwa.
Wakiongea na Bongofive wameeleza namna walivyokuwa wanazisubiria jezi hizo kwa hamu kubwa
Simba imetambulisha jezi zao leo tarehe 7/8/2022 siku moja kabla ya siku yao kubwa ya Simba day na huenda ndio imechangia mashabiki kufurika wengi.