Habari
Tembo aua watu wawili, mama na mtoto Zimbabwe
Mama na mtoto wake wa miezi kadhaa walikanyagwa hadi kufa na tembo kusini-mashariki mwa Zimbabwe.
Mwanamke huyo, ambaye alikuwa amewatembelea jamaa zake katika wilaya ya Chipinge vijijini wakati wa Sikukuu ya Mwaka Mpya, alikuwa njiani kurudi nyumbani wakati tembo alipowashambulia.
Msemaji wa Mamlaka ya Hifadhi za Zimbabwe Tinashe Farawo alisema kuwa tembo huyo aliwashambulia ghafla na kuwaua wawili hao papo hapo.
Tembo huyo ameuawa.
Migogoro kati ya binadamu na wanyamapori ni ya kawaida katika baadhi ya maeneo ya vijijini nchini Zimbabwe.