Habari

Tetemeko la ardhi laua 56 Indonesia

Watu 56 wamekufa na wengine 700 wamejeruhiwa kufuatia tetemeko la ardhi la 5.6 katika kipimo cha Richiter kulikumba eneo la karibu na mji mkuu wa Indonesia, Jakarta.

Picha za televisheni zimeonyesha uharibifu mkubwa wa mji wa Cianjur, ikiwemo barabara na nyumba zilizoharibiwa vibaya.

Meya wa mji huo Herman Suherman amesema kuna uwezekano idadi ya waliofariki ikaongezeka. Suharyanto, mkuu wa wakala wa kitaifa wa kukabiliana na majanga, amesema wahanga wengi waliangukiwa na vifusi kutoka kwa nyumba zao zilizobomoka.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents