Burudani
Tetesi za uhusiano kati ya Rihanna na Benzema zazidi kukua, waonekana tena pamoja
Mambo yanazidi kupamba moto kati ya Rihanna na mchezaji wa soka wa klabu ya Real Madrid, Karim Benzema.
Wawili hao wameonekana wakila bata pamoja kwenye klabu ya Hollywood usiku wa Jumatatu.
Kwa mujibu wa TMZ wawili hao walionekana wakitoka kwenye kiota cha Henry’s na ingawa kila mmoja alitoka kivyake, ilikuwa wazi kuwa walikuwa pamoja.
Hiyo sio mara ya kwanza wawili hao kukutana katika maeneo ya starehe.