Habari
Tuwe waangalifu katika kuchagua Barakoa, msifikiri tunapendwa mno- Rais Magufuli (+Video)
Serikali haijakataza barakoa lakini tuwe waangalifu katika kuchagua barakoa ipi ninavaa, tutaangamia vita ya kiuchumi ni mbaya, namuona mama pale ameshona yake ya kitenge hongera sana.
Corona itakwisha, mwaka jana tulipita salama mpaka watu wakawa wanatushangaa, hata Marais wenzangu wakawa wananiambia nyinyi ni wachawi huko Tanzania nikasema Mchawi ni Mungu, tulipita wapo walioathirika kidogo lakini tulipita na sasa tutapita.
Watu wangefurahi hata Watanzania wote wakifa, mnaweza hata kuletewa barakoa zenye Corona, unaivaa kumbe unapata Corona ili ukawaambukize Watanzania wengine, ni lazima tutumie busara kwa barakoa tunazozivaa” JPM