Burudani

Tuzo za Watu 2015: Ukweli kujulikana leo usiku, Hyatt Regency Hotel

Baada ya wiki kadhaa za mpambano mkali wa kura za tuzo za watu, leo ndio fainali.

TUZO ZA WATU Logo black background

Majina matatu yanashindania tuzo kwenye vipengele 13 vya mwaka huu. Majina hayo yameingia baada ya kuvuka michujo miwili migumu. Ni kura za mashabiki peke yake ndio ziliwaingiza kwenye fainali hiyo na mshindi atapatikana kwa kura za wananchi, hakuna kingine.

Washereheshaji kwenye fainali hizo ni Vj Penny na mchekeshaji Dogo Pepe huku muimbaji wa kike anayechipukia kwa kasi Ruby akitarajiwa kutumbuiza.

“Watu wategemee performance nzuri kutoka kwangu,” amesema Ruby. “Kama kawaida mimi napenda muziki mzuri na itakuwa ni live performance. So wategemee kizuri na hali ya hewa ya muziki na yenyewe itabadilikabadilika kutoka kwa Ruby.”

“It’s finally here. The 2nd annual Tanzanian People’s Choice Awards,” ameandika Mwenyekiti Mtendaji wa Bongo5 Music Group, Luca Neghesti kwenye Instagram.

“Wananchi wamepiga kura kwa wingi na washindi wenye kura nyingi zaidi wamepatikana, kazi iliyobaki ni kujua majina yao na kuwakabidhi tuzo leo usiku. Hongera nyingi sana kwa nominees wote, kupendekezwa na kufika hatua ya kupigiwa kura ina maanisha kwamba mnakubalika na jamii!!! #tzw2015 #TuzoZaWatu Raha.com watawezesha show kuonekana live kupitia bongo5.com,” ameongeza.

Haya ndio majina yaliyoingia kwenye fainali

Mtangazaji wa redio anayependwa

D’Jaro Arungu – TBC FM
Maryam Kitosi – Times FM
Millard Ayo – Clouds FM

Kipindi cha redio kinachopendwa

Amplifaya – Clouds FM
Hatua Tatu – Times FM
Papaso – TBC FM

Mtangazaji wa runinga anayependwa

Abdallah ‘Dullah’ Ambua – EATV
Salama Jabir – EATV/Maisha Magic
Salim Kikeke – BBC Swahili

Kipindi cha runinga kinachopendwa

In My Shoes – EATV
Mkasi – EATV
Planet Bongo – EATV

Blog/Website inayopendwa
Hassbabytz.com
Millardayo.com
timesfm.co.tz

Muongozaji wa video anayependwa
Adam Juma
Hanscana
Nisher

Muongozaji wa filamu anayependwa

JB
Leah Mwendamsoke
Vincent ‘Ray’ Kigosi

Muigizaji wa kike wa filamu anayependwa

Jacqueline Wolper
Riyama Ally
Wema Sepetu

Muigizaji wa kiume wa filamu anayependwa

Hemedy PHD
JB
King Majuto

Mwanamuziki wa kike anayependwa TZW10

Lady Jaydee
Linah
Vanessa Mdee

Mwanamuziki wa kiume anayependwa

Alikiba
Barnaba
Diamond Platnumz

Filamu inayopendwa

Chausiku
Kigodoro
Madam

Video ya muziki inayopendwa

Nani kama Mama – Christian Bella f/ Ommy Dimpoz
Wahalade – Barnaba
XO – Joh Makini

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents