Habari
Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania umetoa wito kwa raia wake kurejea Marekani kisa Corona
Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania umetoa wito kwa raia wake kurejea Marekani, kufuatia uwepo wa maambukizi ya virusi vya #COVID19. Wote wanaotaka kuondoka wametakiwa kufanya hivyo mapema kwani hadi kufikia Machi 29, 2020 Shirika la Ndege Ethiopia litakuwa shirika pekee lenye ndege za kutoka nje ya Tanzania.