Bongo5 ExclusivesBurudaniHabari

Unahisi Marioo hakustahili tuzo yoyote?? kama ndio au hapana tupe sababu

Kupitia kipindi cha RECAP NA MANDO @el_mando_tz ameanzisha mjadala juu ya msanii wa muziki wa Bongo Fleva kukosa tuzo yoyote kwenye tuzo za TMA.

@el_mando_tz ameeleza kuwa kwa maoni yako hakuona kama Marioo alikuwa ni msanii wa kukosa tuzo maana amefanya vizuri zaidi hata kuliko baadhi ya wasanii waliopata tuzo.

@el_mando_tz ametolea mfano ngoma (Nyimbo) za Marioo ambazo anahisi zimefanya vizuri zaidi na zilistahili kupata tuzo walau moja, hata kama sio tuzo basi msanii kwa namna alivyofanya vizuri angepata tuzo.

Ametoa mfanno wa ngoma hizo kama NAOGOPA aliyomshirikisha Harmonize, Dear EX, Beer TAMU ambazo kwa upande wake anaamini kwa mwaka 2022 zilifanya vizuri sana.

Vipi kwa upande wako, unahisi Marioo Hakustahili tuzo kwa mwaka 2022?? kama alistahili tupe sababu na kama hakustahili tupe sababu pia.

 

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents