Siasa
Uteuzi na utenguzi wa Rais, Ally Hapi RC Mara, Luhumbi RC Mwanza Chalamila atenguliwa
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko madogo ya Wakuu wa Mikoa na kuteua wengine ambapo Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhandisi Robert Luhumbi anahamia Mkoa wa Mwanza na aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Mwanza Albert Chalamla uteuzi wake umetenguliwa huku Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ally Hapi akihamishiwa mkoani Mara.