Habari
VIDEO: Rais Samia Suluhu kuhutubia Bunge la Kenya
Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kufanya ziara rasmi ya siku mbili nchini Kenya kuanzia tarehe 04 Mei 2021 kwa mwaliko wa Rais Uhuru Kenyatta. Akiwa nchini Kenya Rais Samia Suluhu atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake Rais Kenyatta na kisha atalihutubia Bunge la Kenya litakalojumuisha Wabunge wa Mabunge yote mawili ya nchi hiyo. Aidha Rais Samia atahudhuria na kuhutubia mkutano wa jukwaa la wafanyabiashara wa Kenya na Tanzania utakaofanyika Jijini Nairobi kwa lengo la kujadiliana masuala mbalimbali yahusuyo fursa za biashara na uwekezaji zilizopo Tanzania na Kenya.