Habari
Vikwazo kutoka nchi za Magharibi havituathiri kitu – Urusi
Urusi imesema vikwazo vya nchi za magharibi havina athari kwake na imeapa kujibu kwa namna yake kufuatia ripoti kwamba Umoja wa Ulaya pamoja na Marekani zinatayarisha vikwazo vipya dhidi yake.
Msemaji wa serikali ya Urusi Dmitry Peskov amesema wale wanaotegemea vikwazo wanapaswa kutafakari tena na wajiulize je, wanatimiza lengo lolote kwa kuendelea na sera kama hiyo ?