Siasa

Vituo viwili vya habari Senegal vyafungwa kisa kuonyesha maandamano (+ Video)

Mamlaka nchini Senegal zimesitisha matangazo ya vituo viwili vya televisheni za kibinafsi baada ya kuzilaumu kwa kuangazia zaidi maandamano yaliyosababishwa na kukamatwa kwa kiongozi wa upinzani, Ousmane Sonko.

Vituo viwili vilivyoathirika na uamuzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Matangazo nchini humo ni Sen TV na Walf TV.

Vituo hivyo vimeshutumiwa kwa upeperushaji wa picha zinazoonesha maandamano baada ya Bwana Sonko kukamatwa, Shirika la habari la AFP limeripoti.

Siku ya Alhamisi, polisi walikabiliana na wafuasi wa Bw. Sonko mjini Bignona kusini mwa eneo la Casamance.

Serikali imethibitisha kuwa mtu mmoja aliuawa siku ya katika ghasia za Alhamisi zilizotokana na kukamatwa na Bw. Sonko mjini Dakar mapema siku hiyo.

Bw. Sonko amelaumiwa kwa kumbaka mwanamke mmoja katika saluni ambako alikwenda kusingwa.

Bofya hapa chini kutazama.

https://www.instagram.com/tv/CMEt8q0BMrp/

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents