
Hotuba ya Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa kuhusu hali ya taifa hilo kwa mwaka 2023 ilikatizwa na dhihaka kutoka kwa chama kimoja cha upinzani na kusababisha ghasia bungeni mjini Cape Town.
Aliposimama kuanza hotuba kundi la wabunge lilijaribu kuzima hotuba yake, kabla ya kutakiwa kuondoka ndani ya bunge.

Kundi la wabunge wa chama cha Economic Freedom Fighters (EFF) wakiongozwa kingozi wao Julius Malema walijaribu kuvamia jukwaa, huku baadhi yao wakiwa wamebeba mabango, na kulazimika kuondolewa nje na walinzi katika moja ya matukio ya kutatanisha.
Utulivu ulivyopatikana, hotuba iliendelea.