HabariSiasa

Wakuu wa mikoa 9 wameteuliwa, 7 wamehamishwa vituo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa wakuu wa mikoa wapya tisa na kuwahamisha vituo vya kazi wakuu wa mikoa 7 na wengine 10 kubakia kwenye nafasi zao.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Taarifa ya Ikulu iliyotolewa usiku wa kuamkia leo Julai 28, 2022 imeeleza kuwa Rais Samia amemteua Albert Chalamila kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera. Chalamila amewahi kuwa Mkuu wa mkoa wa Mbeya na Mwanza.

Aidha Rais Samia amemteua Dk. Yahaya Nawanda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu akichukua nafasi ya David Kafulila. Kabla ya uteuzi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora.

Pia Rais Samia amemteua Dk. Raphael Chegeni kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara akichukua nafasi ya Ally Hapi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents