Walimu zaidi ya 25 wa Shule ya Sekondary ya Aga Khan Mzizima Upanga Dar Es Salaam amegoma kufundisha na kujifungia ofisini kwa madai wamekuwa wakibaguliwa na viongozi wa shule hiyo ambao wanadaiwa kuwa ni Wahindi.
Walimu hao wamedai wanafanya kazi katika mazingira ya wasiwasi baada ya wenzao zaidi ya 15 kufukuzwa bila sababu za msingi na nafasi zao kuchukuliwa na Wahindi.
Bongo5 iliutafuta uongozi wa shule hiyo na kukataa kuzungumzia tuhuma hizo huku wakidai tayari wameshaanza mazungumzo na walimu hao kutatua changamoto zilizojitokeza.