
Wanasayansi wameunda chanzo cha nishati ambacho kinaweza kuruhusu wanaanga kuishi kwenye Mwezi kwa muda mrefu. Mpango wa Artemis unaoongozwa na Nasa unatarajia kuweka kituo cha nje cha Mwezi kufikia karibu 2030.
Chuo Kikuu cha Bangor kimeunda seli za mafuta ya nyuklia, zenye ukubwa wa uwa la waridi ili kutoa nishati inayohitajika kuendeleza maisha huko. Profwsa Simon Middleburgh kutoka chuo kikuu alisema kazi hiyo ilikuwa changamoto – “lakini imekuwa ya kufurahisha”.
Mwezi, ambao pia unajulikana na wengine kama lango la Mars, una rasilimali nyingi muhimu zinazohitajika kwa teknolojia ya kisasa. Matumaini ni kwamba inaweza kutumika kama njia ya kufikia sayari zaidi