Bongo5 ExclusivesBurudaniHabariMahojiano
Wasanii waliofanya vizuri jukwaani mwaka 2022
Baada ya wasanii kadhaa kufunga mwaka kwa kufanya show kadhaa maeneo tofauti ya hapa nchini, @el_mando_tz kwenye kipindi chake cha Recap na Mando ameitaja show ya @mbosso_ kuwa ndio show bora ya kufungia mwaka.
Mbali na hilo @el_mando_tz amemtaja @rayvanny kama ndio msanii aliyefanya vizuri kwenye show zake zote kwa mwaka 2022 zikiwemo za FIESTA kwa namna ya ubunifu wake.
@el_mando_tz amezitaja baadhi ya show za @rayvanny ikiwemo ya Sumbawanga aliyoingia kama mganga wa kienyeje, show ya Tabora aliyoingia na gari Semi-trella laini pia show ya Dar Es Salaam zote za Fiesta aliyopanda na vifaa vyq kwenda mwezini.
Mbali na @el_mando_tz wewe unahisi msanii gani amefanya vizuri jukwaani kwa mwaka 2022??