Habari
Waziri Bashungwa alivyotoa sababu za kufunguliwa Online Tv na sio Magazeti (+ Video)
Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo @innocentbash amewaagiza TCRA kuzifungulia Online TV zote ambazo zilifungiwa, huu ukiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan alilolitoa hapo jana.
“Mpaka sasa tuna TV za Mtandaoni (Online TV) 440 ambazo tumezisajili, kwa kushirikiana na Waziri mwenzangu wa Mawasiliano (Ndugulile) nimetoa maelekezo Online TV zote ambazo zilizuiwa zianze kufanya kazi lakini ni kwa kufuata masharti kama ya usajili, Magazeti yaliyofungiwa tutaenda nayo case by case, Ofisi yangu iko wazi, waje tuangalie nini kilipelekea kufungiwa na nini kifanyike ili warudi kwenye utaratibu wa kuendesha Vyombo vya Habari kwa mujibu wa sheria na kanuni za uendeshaji wa Vyombo vya Habari”