Habari

Waziri Mkenda atia mkazo sera ya Elimu 2023

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, Aprili 11, 2025, amefungua rasmi Mkutano wa 35 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo mkoani Morogoro, na kutoa wito kwa watumishi kuhakikisha wanasimamia kikamilifu utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo Toleo la 2023.

Amesema sera hiyo inalenga kuleta mageuzi ya kimfumo katika sekta ya elimu kwa kutoa maarifa na ujuzi unaohitajika katika karne ya 21, kupitia mikondo miwili ya elimu, Elimu ya Jumla na Elimu ya Amali, ili kumpa kila mwanafunzi fursa ya kuchagua njia inayomfaa kwa maisha na taaluma.

 

 

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents