Michezo
Yanga walazimishwa sare na Polisi Tanzania
Goli la Pius Boswita dakika ya 90 linaipatia pointi moja Polisi Tanzania mbele ya Yanga SC kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.
FT : Polisi Tanzania 1 – 1 Yanga SC. Yanga imeruhusu bao hilo dakika za majeruhi kabisa wakati ambao baadhi ya mashabiki wengi wa #yangasc wakiamini mpira umekwisha na wanaondoka na alama tatu muhimu ili kujiimarisha zaidi kileleni.
Yanga imekuwa katika kipindi kisicho kizuri kwa matokeo ya hivi karibuni #vpl kwani kabla ya leo wiki iliyopita Wananchi walijikuta wakiacha pointi tatu muhimu pale Uwanja wa Mkwakwani baada ya kufungwa magoli 2 – 1 dhidi ya Coastal Union.