Zaidi ya MILIONI 80 zawekwa kwenye shindano la Pooltable
ZAIDI YA MILIONI 80 ZAWEKWA KWENYE SHINDANO LA POOLTABLE
Leo tarehe 05/08/2025 Klabu ya Cue
Master Billiard Center kwa kushirikiana na
Cue sports Bar&Lounge kinawatangazia
mashindano ya Mchezo wa Pooltable Afrika yatakayofanyika hapa katika Klabu ya Cue Masters Billiards iliyopo Manzese Argentina jijini Dar Es Salaam,Shindano litahusisha Vilabu na mchezaji mmoja mmoja kwa Wanaume na Wanawake kutoka Mataifa 10 ya Afrika.

Akizungumza Mkurugenzi wa Cue Master,
Timar Mtengo alisema mashindano hayo
yanatarajiwa kuanza tarehe 08/08/2025 na
kumalizika tarehe 11/08/2025 hapa hapa
katika Klabu ya Cue Master Billiards Center
Mtengo alizitaja Nchi zilizothibitisha
kushiriki ni Afrika Kusini, Zambia, Malawi,
Kenya, Uganda,Zimbabwe, Sudani
kusini,Eswetin,Botswana na Wenyeji
Tanzania.




