Ziara ya kwanza ya Biden nje ya Marekani
Rais Joe Biden ameanza ziara yake ya kwanza ya kigeni tangu aingie madarakani kwa kusifia kujitolea kwa Marekani katika jumuiya ya kujihami ya NATO na kutuma onyo kali kwa Urusi wakati akiwa Uingereza
Biden amesema amedhamiria kuyajenga upya mahusiano ya Marekani na Ulaya na kurekebisha mahusiano na Urusi baada ya miaka minne migumu chini ya Rais Mrepublican Donald Trump, ambaye maamuzi yake ya kuongeza ushuru kwa bidhaa na kujiondoa kwenye mikataba yaliharibu mahusiano na washirika wakuu. Biden atakuwa Uingereza hadi Jumapili
Kwa washirika wengi wa Marekani, Biden ni kiongozi wanayemtazama kwa jicho la faraja. Na sababu kubwa ni kwamba mtangulizi wake alisababisha mvurugano mkubwa mara kwa mara, akiushutumu muungano wa kijeshi wa NATO kwamba umekuwa ukiitumia vibaya Marekani, na kuitukana Umoja wa Ulaya, na wakati mmoja kufikia hatua mpaka ya kuondoka kwenye mkutano wa kilele wa G7 uliofanyika Canada mwaka 2018.