FahamuHabari

Zifahamu ajali mbaya zaidi kuwahi kutokea Tanzania

Ajali ya ndege ya Precision Air iliyotokea Bukoba, nchini Tanzania na kuua watu 19, ni moja ya ajali nyingi zinazotokea katika maeneo mbalimbali.

Mkaguzi Mkuu wa Ajali za Ndege nchini humo, kutoka Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi, David Nyamwihura aliwahi kunukuliwa na gazeti la Mwananchi nchini Tanzania kwamba, ripoti ya ajali za ndege hapa nchini humo inabainisha kuwa tangu mwaka 1920 hadi 2013 zimewahi kutokea ajali 52 zilizosababisha vifo vya watu 196. Na idadi kubwa ya ajali hizo hutokea maeneo ya milimani.

Lakini ajali ya sasa imetokea katika ziwa Victoria, mita chache kutoka uwanja wa ndege wa Bukoba, wakati ndege ya Precision Air PW 494 ikijiandaa kutua ikitokea Dar es Salaam kupitia Mwanza.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amesema serikali itafanya uchunguzi kubaini chanzo hasa cha ajali hiyo, iliyoibua simanzi kwa watanzania.

Bukoba
Ajali ya ndege ya Precision Air Bukoba ilua watu 19

Pamoja na kwamba ni ajali ya ndege iliyoanguka ziwani, imekumbusha machungu ya ajali nyingi kubwa zilizowahi katika maeneo mbalimbali na kupoteza idadi kubwa ya watu.

Hakuna asiyesahau vifo vya watu zaidi ya 100 walioungua na moto wa mlipuko wa gari la mafuta mkoani Morogoro. Lakini vifo vya wanafunzi zaidi ya 30 wa shule ya Lucky Vincent, Arusha kwenye ajali ya basi dogo iliyotumbukia katika mto Marera ulioko katika mlima Rhotia, Karatu nayo ilileta simanzi kubwa.

Ajali nyingi zimetokea barabarani, angani na majini, lakini hizi tano zitaendelea kukumbukwa zaidi nchini Tanzania.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents