Habari
Waziri Nape akerwa Dada anayelala na Nyoka na kufanya nae mapenzi
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye, ameonesha kukerwa na habari iliyowekwa mtandaoni yenye mahojiano na Mwanamke Mtanzania anayedai kuishi na nyoka pamoja na kufanya nae mapenzi.
Akiongea katika Kongamano lililoandaliwa na Jukwaa la Wanahabari wa Mitandao ya Kijamii (JUMIKITA) May 21 2024, Waziri Nape amenukuliwa akisema “juzi blogu moja imerekodi Dada mmoja anasema unajua mimi huyu nyoka huwa nalala nae kupata pesa alafu Mtu mzima unarekodi una-publish, tunataka tuwaambie nini Watoto wetu?”
“Hata kama tunatafuta viewers kaa kwenye viatu vya yule unayemuhudumia” ——— Waziri @NapeNnauyeW