Burudani
Mr. Puaz aeleza A-Z sakata la msanii wake Harmonize kushindwa kutumbuiza Kenya ‘mapromota walitutelekeza hotelini’ (+AUDIO)
Meneja wa Harmonize, Mr. Puaz ameeleza A-Z sakata la kuachwa solemba na Mapromota wikiendi iliyopita mjini Eldoret nchini Kenya.
Mr. Puaz amesema kuwa mapromota hao walishindwa kumalizia kiasi kilichobakia kama mkataba wao ulivyotaka, huku yakiwa yamepita masaa kadhaa watu wakimsubiri msanii huyo kupanda jukwaani.