Habari

Dereva wa basi la shule Kenya auawa kwa risasi na majambazi

Dereva wa basi la shule ameuawa kwa kupigwa risasi baada ya majambazi kuvamia msafara wa mabasi matatu huko Marakwet katika eneo la Kerio Valley.

Kulingana na komanda wa polisi kaunti ya Elgeyo Marakwet, baadhi ya wanafunzi na walimu walipelekwa katika hospitali za karibu kupata matibabu huku ikihofiwa kwamba huenda kuna walio katika hali mahututi.

Inasemekana kwamba walimu na wanafunzi walikuwa wanarejea shuleni baada ya kuhudhuria tukio la kitaaluma.

Kulingana na waliofika kuwaokoa, wavamizi hao walimiminia risasi dereva aliyeaga dunia papo hapo kabla ya kuanza kurusha risasi dhidi ya walimu na wanafunzi.

Hata hivyo Seneta wa Elgeyo Marakwet Kipchumba Murkomen ameonekana kuwashutumu Waziri wa mambo ya ndani Fred Matiang’i na Inspekta Jenerali wa Polisi Hillary Mutyambai.

Kwa upande wake Waziri wa mambo ya ndani Fred Matiang’i, ameagiza kukamatwa kwa mwalimu mkuu wa shule hiyo mara moja.

Akizungumza katika tulio kuhusu elimu na washika dau wengine, Matiang’i amelaumu utawala wa shule kwa kukiuka sheria zilizowekwa na serikali kuhusu utumiaji wa mabasi ya shule.

Kwa mujibu wa BBC. Matiang’i ameeleza kuwa serikali iliweka sheria ya kukataza mabasi ya shule kutumika baada ya saa kumi na mbili unusu jioni.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents