Kupitia kwenye kipindi chake cha RECAP & MANDO @el_mando_tz amezungumzia kauli ya @rayvanny ya kupoteza milioni 70.
Mwanzoni @rayvanny hakueleza hizo hela zimepoteaje lakini kupitia alichokifanya Mbeya ikaja kudhihirisha namna alivyopoteza pesa hizo kupitia bwawa alilojenga na baadae kubomoka.
@el_mando_tz anaeleza kuwa inawezekana ni kweli au isiwe kweli @rayvanny kupoteza hicho kiasi cha pesa lakini kitendo cha kujenga bwawa kwa namna ile kwa ajili ya show moja inaonyesha namna gani anajidhihirisha ukomavu wake kwenye muziki.
Kupitia hicho tayari ameonyesha Thamani yake, kwa namna moja ai nyingine muziki wetu umefika mahali pa kujivunia kupitia ubunifu wa wasanii wetu.