Harusi yavurugika baada ya mchepuko wa bwana harusi kujitokeza kanisani
Harusi ya mwanaume mmoja jijini Blantyre, nchini Malawi imeingia doa siku ya jumamosi ya wikiendi iliyopita baada ya mwanamke mmoja kusimama mbele ya kanisa na kudai kuwa bwana harusi ni mchumba wake na alimuahidi kumuoa.
Kwa mujubu wa maelezo kutoka kwa shuhuda wa tukio hilo wameeleza kuwa limetokea katika kanisa la Living Waters Church (LWC), Dayosisi ya Chilimba mjini Blantyre. Ambapo waumini wamesema walishtuka ghafla kumuona mwanamke huyo aliyekuwa amevalia suti akikimbia mbele ya altare baada ya Mchungaji kutangaza kuwa kama kuna mtu anapingamizi ajitokeze kanisani hapo.
Tukio hilo lilianza kusambaa kwenye mtandao wa Twitter baada ya mdau mmoja kurusha picha hizo mtandaoni kabla ya kunaswa na vyombo vya habari.
Another wedding cancelled yesterday after the guys ex stood up in church and said the guy was still her boyfriend. Meanwhile the bride😢😢 pic.twitter.com/W6oXnjSfkv
— MALI OHN (@JMaliKay_27) November 5, 2017
Hata hivyo baada ya tukio hilo kutokea Mchungaji alilazimika kusimamisha zoezi hilo kwa muda lakini baadae Bi. Harusi alirejea na shughuli kuendelea. Ingawaje haijatolewa taarifa rasmi kuhusu mahusiano kati ya Bwana Harusi mwanamke huyo aliyejitokeza kanisani hapo.
Chanzo:Mtandao wa FaceOfMalawi