Burudani
Kuhusu video za muziki zenye maadili, MC Pilipili amtaja msanii mkubwa anayemvutia (+Video)
Mchekeshaji maarufu nchini Tanzania, MC Pilipili amesema kuwa video nyingi za wasanii wa Bongo Fleva hazizingatii maadili ya Mtanzania kwani wahusika kwenye video hizo hususani Wanawake huwa wanakuwa nusu utupu.
MC Pilipili amesema kwa upande wake anavutiwa na Alikiba kupitia wimbo wake wa Seduce Me kuwa ni wimbo bora uliozingatia maadili ya kitanzania na bado video imetazamwa na mamilioni ya watu mtandaoni.
Tazama MC Pilipili akizungumzia ngoma hiyo na maoni yake kuhusu wasanii wanaotoa video zisizozingatia maadili.