Michezo
Man United wakomaa na PSG
![](https://bongo5.com/wp-content/uploads/2024/06/Screenshot-2024-06-26-at-13.07.27.png)
Klabu ya Manchester United ya Ligi Kuu Uingereza inahusishwa kuhitaji saini ya kiungo wa kati wa klabu ya PSG ya Ufaransa na timu ya Taifa Uruguay Manuel Ugarte.
Ugarte ambaye yupo kwenye Kambi ya timu ya Taifa ya Uruguay inayoshiriki michuano ya kombe la mataifa America (Copa America) alionyesha kiwango bora sana kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi dhidi ya Panama, Uruguay ikashinda 3-1.
Ugarte anatajwa kuchukua nafasi ya Casemiro anayetajwa kuhitajika na timu za Saudi Arabia.