![](https://bongo5.com/wp-content/uploads/2022/08/tanzaniapiic-data.jpeg)
Kupitia mitandao yake ya kijamii Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewapongeza raia wa taifa la Kenya kwa kushiriki uchaguzi na kumpata rais wa taifa lao ambaye ni William Ruto.
Rais Samia Suluhu ameandika kuwa: ” Ninapenda kuwapongeza kwa dhati wananchi wa Kenya kwa kushiriki uchaguzi wao mkuu kwa amani na utulivu, ambapo matokeo yake ni Dkt @WilliamsRuto kutangazwa kuwa Rais mteule wa Kenya. Tanzania itaendeleza undugu na ushirikiano wa Kihistoria na Kenya uliodumu miaka na mikaka.”