Rais wa Marekani Donald Trump ajibu mapigo kwa kuikosoa China, baada ya kupandisha ushuru mara dufu bidhaa kutoka Marekani
Rais wa Marekani Donald Trump ajibu mapigo kwa kuikosoa China, baada ya kupandisha ushuru mara dufu bidhaa kutoka Marekani
Rais wa Marekani Donald Trump ametetea vita vya kibiashara kati yake na China wakati hali ya wasiwasi ikiongezeka wakati masoko ya fedha yakizidi kuporomoka huku akiahidi kufikia makubaliano hivi karibuni na rais wa China Xi Jinping.
Kwa mujibu wa DW. Katika mfululizo wa ujumbe alioandika kwenye ukurasa wake wa twitter mapema hii leo Trump ameendelea kuipigia debe kauli mbiu yake ya Marekani Kwanza katika kuunga mkono hatua za kuongeza ushuru dhidi ya bidhaa za China huku akiyataka makampuni ya Marekani kumuunga mkono kwa kuhamisha biashara zao kutoka China. Trump amesema kwa sasa anaweza kufikia makubaliano na Beijing lakini hatakubali tena kuwekewa mbinyo huku akiikosoa China kwa jaribio lake la dakika za mwisho la mazungumzo.
China will be pumping money into their system and probably reducing interest rates, as always, in order to make up for the business they are, and will be, losing. If the Federal Reserve ever did a “match,” it would be game over, we win! In any event, China wants a deal!
— Donald J. Trump (@realDonaldTrump) May 14, 2019
….This money will come from the massive Tariffs being paid to the United States for allowing China, and others, to do business with us. The Farmers have been “forgotten” for many years. Their time is now!
— Donald J. Trump (@realDonaldTrump) May 14, 2019
By Ally Juma.