Samuel Eto’o rais mpya wa shirikisho la soka nchini Cameroon
Mchezaji Nyota wa zamani wa Cameroon Samuel Eto’o amechaguliwa kuwa rais wa shirikisho la soka la Cameroon (FecafootOfficie)
Eto’o, mwenye umri wa miaka 40, ameahidi mageuzi mbalimbali ili kustawi mchezo huo.
“Lazima tuwalete wanasoka katikati ya sera zetu,” alisema baadaye. “Ni jukumu letu kuhakikisha kwamba wale wanaocheza mpira huu wanapata maisha ya staha kutokana nayo.”
Nyota huyo wa zamani wa Barcelona, Inter Milan na Chelsea pia ameahidi kujenga angalau viwanja 10 wakati wa uongozi wake.
“Nimezungumza na jumuiya ya wafanyabiashara na tuna uhakika tutapata wawekezaji wanaofaa ambao wanaweza kuandamana nasi katika kutimiza malengo yetu,” Eto’o alisema kabla ya uchaguzi.
Mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa Samuel Eto’o ataendesha soka la Cameroon kwa miaka minne ijayo baada ya kuchaguliwa kuwa mkuu wa shirikisho hilo siku ya Jumamosi.
Etoo ambaye aliwahi kushinda tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika mara nne alimshinda mpinzani wake Seidou Mbombo Njoya, makamu wa nne wa rais katika Shirikisho la Soka Afrika.
Wagombea saba walipaswa kushiriki uchaguzi, lakini watano kati yao walijiondoa asubuhi ya uchaguzi.
I’ll be remembering today as one of the proudest moments of my life. I’m deeply grateful for to be elected as the new president of @FecafootOfficie. Every vote represents the energy and ambition of our football family to take our beloved sport to a level we’ve never seen before.
Kugombea kwa Eto’o kumeibua hisia za watu wengi kutokana na mkutano huo kutangazwa moja kwa moja kwenye televisheni ya taifa ya Cameroon.
Sasa atakuwa mkuu wa FA ya Cameroon (Fecafoot) wakati nchi hiyo itaandaa Kombe la Mataifa ya Afrika mwezi Januari na Februari.