Antony Joshua amchakaza Povetkin kwa TKO, na huu ndio mkwanja aliyoingiza (+video)
Bondia Mrusi Alexander Povetkin amejikuta akishindwa kuvumilia makonde mazito ya Muingereza Anthony Joshua baada ya kukubali kipigo cha TKO katika raundi ya 7 ya pambano lao kali la ubingwa wa dunia uzito wa juu.
Povetkin akionekana ni hatari kunako raundi ya kwanza alirusha konde kali lililomtoa Joshua damu puani. Jambo ambalo lilizua hofu kwa mashabiki wa bondia huyo waliohudhuria kwenye pambano hilo kunako dimba la Wembley .
Hata hivyo, Joshua baadae akaendelea kujilinda zaidi hadi raundi ya 7 alipofanikiwa kumpiga TKO na kunyanyua mkanda wa ubingwa wa dunia wa uzito wajuu.
Kwa ushindi huo, Joshua amefanikiwa kuchukua kiasi cha £uro milioni 20 sawa na Bilioni 54 za Kitanzania huku mwenzie akichukua Euro Milioni 6.
https://youtu.be/kqHGHozsXgM