Burudani

Baada ya kufungiwa na Bodi ya Filamu, mrembo Wema Sepetu apigwa rungu lingine tena

Ikiwa ni siku tatu zimepita tangu Bodi ya Filamu nchini Tanzania, itangaze kumfungia Muigizaji wa filamu Wema Sepetu kutojihusisha na tasnia hiyo, kwa mara nyingine leo amefungiwa tena na Chama cha Waigizaji Kinondoni.

Related image
Wema Sepetu

Chama cha Waigizaji Wilaya ya Kinondoni (TDFAA) kimemfungia Mwanachama wake Wema Sepetu kujihusisha na masuala ya filamu kwa miaka miwili, kufuatia muigizaji huyo kusambaza picha na video zake za faragha kwenye mitandao ya kijamii.

Hii si mara ya kwanza kwa Wema kufanya mambo ya ajabu, aliwahi kuanika video ya makalio tukamuita akaomba radhi.“amefunguka Msemaji wa chama hicho, Masoud Kaftany kwenye taarifa aliyoitoa kwenye vyombo vya habari.

Kwa upande mwingine, Chama hicho kimezitaka Mamlaka za Serikali zipuuze utetezi wa Wema kwa kudai kuwa una lengo la kuzipumbaza zisimchukulie hatua.

Wema Sepetu Alhamisi ya wiki iliyopita Oktoba 25, 2018 alijitokeza hadharani kuomba radhi kwa Watanzania kufuatia video zake za faragha kusambaa mitandaoni.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents