Burudani
Busy Signal amvisha nyota Robert Mugabe kwenye wimbo wake mpya, adai ndio wakombozi wa kweli Afrika (+video)
Msanii wa muziki wa Reggae kutoka Jamaica, Busy Signal ameachia wimbo mpya unaokwenda kwa jina la ‘Great Men’ ambapo ametaja majina ya viongozi wa zamani waliowahi kufanya mageuzi kwenye nchi zao, akiwemo Nelson Mandela.
Kwenye mstari uliomlenga Rais wa zamani wa Zimbabwe, Robert Mugabe, Busy amesema “Acha tuwaongelee watu wetu waliopigania haki zetu”
Lakini cha kushangaza mkali huyo wa Reggae hajamtaja kabisa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere ambaye kwa namna moja ama nyingine ndiye aliyezisaidia nchi za Zimbabwe na Afrika Kusini kupata uhuru.