Burudani
Dar Es Salaam kujengwa ukumbi wa kisasa unaoingiza watu elfu 20, Wasanii wapigwa onyo (+video)
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Mhe. Paul Makonda ameahidi kujenga ukumbi wa kisasa Jijini humo, utakaokuwa na uwezo wa kuingiza watu 20,000 .
RC Makonda akiongea kwenye mkutano wake na wasanii wa muziki na Waigizaji, jana Januari 31, 2019 ametoa ahadi hiyo, huku akiwaonya Wasanii kutumia umaarufu wao vizuri na sio kuanza kujiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya na vitu vingine vinavyoiharibu jamii.