Habari
Dudu Baya apwata na janga lingine zito
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limetangaza kufuta usajili wa Msanii, Godfrey Tumaini maarufu kama Dudubaya kuanzia jana Februari 28, kutokana na utovu wa nidhamu.
Barua hiyo iliyosainiwa na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Godfrey Mngereza amesema kuwa baraza limechukua hatua hizo baada ya msanii huyo kukamatwa na jeshi la polisi kutokana na kauli zake kwenye mitandao ya kijamii.
Kwa sasa Dudu Baya anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika kituo cha Oyster-bay jijini Dar es salaam kwa kosa la uhalifu mtandaoni.