Burudani

Harmonize atangaza balaa lingine na Wizkid

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Harmonize ametangaza kuachia kolabo nyingine wiki ijayo na msanii kutoka Nigeria, Wizkid.

Harmonize na Wizkid

Harmonize ambaye wiki hii alikuwa nchini Australia kikazi kwenye tamasha la AfroEast, Amethibitisha kolabo hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram na kuahidi kuwa inatoka wiki lijalo.

Tamasha la AfroEast limetumbuizwa kwa siku mbili katika miji ya Sydney na Melbourne nchini Australia na mastaa wengine waliotumbuiza kutoka Afrika ni Wizkid na Yemi Alade.

Hii inakuwa ni kolabo nyingine kubwa ya Harmonize kufanya na msanii mwingine kutoka Nigeria, Baada ya kufanya kolabo na Yemi Alade, Burna Boy, Timaya na wengineo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents