Habari
Mhe. Ngeleja, Nape Nnauye, Juma Nkamia wateuliwa
Mbunge wa jimbo la Sengerema kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Wiliam Ngeleja ameteuliwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai kuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwenye kamati ya kudumu ya Bunge ya kipindi cha 2018 hadi 2020.
Wabunge wengine waliyoteuliwa kwenye kamati hiyo ni Mhe. Nape Nnauye mbunge wa Mtama, Andrew Chenge, Hawa Ghasia na wengineo,soma zaidi kwenye orodha ya wabunge wote waliyoteuliwa kwenye kamati hiyo.