Migos watangaza ujio wa ‘Culture II’
Kundi la Rap linalofanya vizuri kwa sasa Migos, kutoka Marekani wanatarajia kuachia albamu yao ya Culture II ifikapo Januari 26 mwaka huu.
Migos linaloundwa na vijana watatu ambao ni Quavo, Takeoff, na Offset waliachia album ya Culture I Januari 27 mwaka uliopita. Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter wamepost kava ya albamu hiyo na kuandika “C U L T U R E I I ”
C U L T U R E I I 👀 pic.twitter.com/pbXJxNB9Am
— MIGOS™ (@Migos) January 16, 2018
Curture II inatarajiwa kuna na ngoma kadhaa ikiwemo ‘MotorSport’ inayofanya vizuri katika chat zambalimbali za muziki ikiwemo Billbords Hot 100 ambapo inashika namba 8, huku ngoma ya ‘Stir Fry ‘ waliofanya na Pharrel inatarajiwa kuwepo.
Albamu ya Culture I, ilikuwa albamu ya kipekee kwani iliweza kufika namba moja kupitia chat za Billboard 200, kwa muda wa wiki moja tokea kuachiwa kwake Januari 27, 2017 na ilifanikiwa kuingia katika kinyang’anyiro cha tuzo za Grammy.